NDUGU wazee, Msahafu wa Waislamu unasema: Likulli Ajalin Kitabu. Mwingereza mmoja kaitafsiri aya hiyo hivi: To Every Age Its Book; yaani Kila Zama na Kitabu Chake. Na sisi wana CCM tunakubali kuwa kila zama ina mwongoizo wake. Azimio la Arusha ni mwongozo wetu wa msingi. Ni dira inayoongoza mwelekeo wa jamii yetu lakini tafsiri zake ni lazima zirekebishwe kila inapohitajika